Loading...

BREAKING NEWS: RAIS MAGUFULI ATAFUNA MFUPA ULIOMTOA JASHO KIKWETE



RAIS John Magufuli ameweka rekodi mpya ya kulipa deni la taifa ambayo haikuwahi kufikiwa katika kipindi cha miaka 12 iliyopita.

Katika rekodi yake hiyo mpya, Rais Magufuli amefanikiwa kulipa deni la taifa la ndani na nje ya nchi katika kipindi kifupi cha miezi mitatu kwa kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa na mtangulizi wake, Rais Jakaya Kikwete, katika kipindi chote cha miaka 10 aliyokaa madarakani.

Kwa mujibu wa taarifa ya hali ya uchumi wa taifa iliyotolewa jana mbele ya waandishi wa habari na Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu ofisini kwake Dar es Salaam, Rais Magufuli amelipa shilingi bilioni 99 za deni la ndani na amelipa pia Dola za Marekani milioni 90 za deni la nje kwa muda wa siku 90.

Taarifa hiyo ya Gavana Ndulu inaonyesha kuwa kasi hiyo ya ulipaji deni la taifa kwa fedha za ndani ambalo hivi sasa limefikia shilingi trilioni 51 haijawahi kufikiwa kipindi chote cha Serikali ya awamu ya nne.

“Serikali imelipa Dola za Marekani milioni 90 kwa deni la nje ambazo ni sehemu ya Dola za Marekani bilioni 600 zilizokopwa Benki ya Stanbic na imelipa pia shilingi bilioni 99 za deni la ndani.

“Ninaposema limelipwa si kwamba Serikali haikopi kabisa, hapana, kinachofanyika kwa sasa fedha zinazokopwa ni ndogo kuliko zile zinazolipwa tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

“Utaratibu huo wa ulipaji uliwahi kutokea kati ya mwaka 2003 na 2004 na unaweza kupunguza kasi ya kuongezeka deni la taifa,” alisema Gavana Ndulu.

Katika mkutano huo, Gavana Ndulu alizungumzia pia mwenendo wa ukuaji uchumi kwa nusu mwaka unaoanzia Januari mpaka Juni 2016 kwa kueleza kuwa ukuaji wa pato la taifa umeongezeka hadi kufikia asilimia 6.7 ikilinganishwa na asilimia 5.7 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2015.


Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright Mwanga Mpya | Designed By BAKI NASI
Back To Top