TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imesema iko katika hatua za mwisho kukamilisha uchunguzi dhidi ya waliokuwa wakurugenzi wa idara sita za Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Akizungumza na Nipashe katikati ya wiki iliyopita mjini Kibaha, Mkurugenzi wa Takukuru, Valentino Mlowola, alisema taasisi inakaribia kukamilisha upelelezi wa suala hilo, baada ya wakurugenzi hao kusimamishwa na bodi ya wakurugenzi ya NSSF kwa tuhuma kadhaa, ikiwamo matumizi mabaya ya ofisi, Julai.
Mbali na wakurugenzi hao, bodi hiyo iliyokaa Julai 15 pia iliwasimamisha mameneja watano na mhandisi mmoja.
Mlowola ambaye ni Kamishna wa Polisi alikuwa akizungumza na Nipashe mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi wa Mahakama ya wilaya, uliofanywa na Waziri Mkuu, Kassimu Mjaliwa.
"NSSF ni mali ya umma na hivyo Watanzania watajulishwa hatua zozote zitakazofikiwa," alisema Mlowola baada ya kuulizwa hatua ambayo uchunguzi wa Takukuru umefika zaidi ya siku 60 tangu upelelezi uanze.
“NSSF ni mali ya umma, tunaendelea na uchunguzi wetu na iwapo kutakuwa na jinai yoyote, hatua stahiki zitachukuliwa na umma utajulishwa kupitia vyombo vya habari.”
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara, alipoulizwa na gazeti hili kuhusu suala hilo hivi karibuni, alisema uchunguzi unaendelea kwa ushirikiano wa karibu na Takukuru.
Alisema baada ya kukamilika kwa uchunguzi huo, umma utajulishwa kuhusu hatua stahiki zitakazochukuliwa dhidi ya wakurugenzi na mameneja waliosimamishwa.
Kikao cha Bodi ya Wakurugenzi ya mfuko huo kilichofanyika Juni 15, mwaka huu, chini ya uenyekiti wa Profesa Samweli Wangwe, kiliwasimamisha kazi wakurugenzi hao kwa tuhuma za kutofuata kanuni, sheria na taratibu katika uwekezaji, usimamizi wa miradi, manunuzi ya ardhi na ajira.
Waliosimamishwa ni Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi, Yacob Kidula, Mkurugenzi wa Fedha, Ludocick Mrosso na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala, Chiku Matessa.
Wengine ni Mkurugenzi wa Udhibiti Hasara na Majanga, Sadi Shemliwa, Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Mahesabu ya Ndani, Pauline Mtunda na Mkurugenzi wa Uendeshaji, Crescentius Magori.
Mameneja waliosimamishwa ni Meneja wa Utawala, Amina Abdallah, Meneja wa Uwekezaji, Abdallah Mseli na Meneja wa Miradi, Mhandisi John Msemo.
Wengine ni Mhasibu Mkuu, Davis Kalanje, Meneja Kiongozi kwa mkoa wa Temeke, Wakili Chedrick Komba na Meneja Mradi, mhandisi John Ndazi.
Uamuzi huo wa kuwasimamisha watendaji hao ulichukuliwa kutokana na taarifa za ukaguzi wa hesabu na shughuli za uendeshaji wa mfuko huo.
Kabla ya hatua hiyo ya bodi, Rais John Magufuli alitengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF wa zamani, Dk. Ramadhan Dau Februari 16 na kumteua kuwa balozi. Amepangiwa kwenda nchi ya Singapore mwezi huu.
Utenguzi wa Dk. Dau ulikuja siku chache baada ya taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuonyesha palikuwa na ukiukwaji wa taratibu katika miradi ya kadhaa ya NSSF.
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out



Post a Comment